BOMU LAOKOTWA MAKABURINI MKOANI MTWARA
Hili ni bomu ambalo jioni ya June 16, 2014 liliokotwa
na watoto waliokua wakicheza karibu na eneo la makaburi kwenye kijiji cha
Mdui kata ya Mawala wilaya ya Mtwara vijijini kwenye mkoa wa Mtwara.
Taarifa ilitolewa
Polisi baadae ambapo baada ya wataalamu kuja na kuchunguza waligundua ni bomu
la kurusha kwa mkono ambalo lina namba TNT MORTAR BOMB 60MM, LOT SOL 618 ambapo
Polisi kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi walichukua hatua za kiusalama na
kwenda kulilipua porini.
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Kaimu kamanda wa Polisi Mtwara Maisha Maganga ameongea na na
kusema ‘ukiliangalia ni bomu ambalo ni la muda mrefu nadhani ni kipindi kile
cha vita ya Msumbiji, tulilipeleka porini likalipuliwa na ulipuaji wake haukuwa
na madhara… na sio kwamba ni bomu tunaweza kusema limeletwa ama imekuaje, ni
bomu la muda mrefu tu’
Post a Comment