AL SHABAAB YADAI NDIO WALIOUA WATU 14 KENYA
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Wanamgambo wa Al Shabaab wamesema kuwa ni wao waliotekeleza
shambulizi Kaskazini Mashariki mwa Kenya ambapo watu 14 waliuawa usiku wa
kuamkia jumanne. Shambulio
hilo linaaminika kuwalenga wafanyikazi wa machimbo ya mawe wasiokua wenyeji wa
mkoa huo. Walioshuhudia
wameambia BBC kuwa walisikia mwanzo milipuko miwili kisha ikafuatiwa na milio
ya risasi.Shirika la msalaba
mwekundu linaongoza oparesheni ya kuwaokoa majeruhi ambao idadi kamili
haijulikani .
Nani washambuliaji ?
Wanamgambo wa Al
shabaab wamekuwa wakilenga wakaazi wasio wenyeji wa asili katika eneo hilo
katika mashambulio yaliyotangulia. Shambulio kama hilo
dhidi ya wachimba migodi lilitokea jijini Mandera mwezi Disemba 2014, ambapo
takriban watu 36 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Marudio ya shambulio
Mashambulio kama haya
yametishia kudumaza shughuli za maendeleo na kiuchumi katika eneo la Kaskazini
Mashariki mwa Kenya ambapo wengi wa wafanyikazi wake ni watu kutoka maeneo
mingine ya Kenya. Wafanyikazi hawa
wamekuwa wakidai kutishiwa maisha, na wengi wa wafanyikazi kama vile walimu na
hata wahudumu wa afya wamesusia kurejea kazini katika eneo hilo wakidai
kutishiwa maisha yao.
Chini
ya siku kumi zilizopita serikali ya Kenya iliondoa marufuku ya kutoka nje
kuanzia magharibi hadi alfajiri, kufuatia wito kutoka kwa viongozi wa kiislamu
waliodai kuwa marufuku hiyo inahujumu ibada za waislamu za usiku katika mwezi
wa Ramadhani. Asili
mia kubwa ya wakaazi katika eneo la kaskazini mashariki mwa Kenya, ni waislamu
wa asili ya kisomali.
Post a Comment