YALIYOJIRI KWENYE MAPOKEZI YA GODBLESS LEMA JIJINI ARUSHA LEO
Maelfu ya wananchi wakiwa katika msafara mrefu zaidi ya pikipiki 500 na
magari ulianzia Uwanja wa Ndege KIA mara baada ya Mbunge huyo kuwasili
uwanjanai hapo majira ya saa 4:20 Asubuhi.
Wafuasi wa Lema wakishangilia barabarani wakati Mbunge huyo akipita.
Mbwembwe za waendesha pikipiki wengine ziliwashinda na kuanza kuanguaka.
Furaha hiyo ilikuwa kwa kilu aliye Mwanachadema
Skafu na vitru mbalimbali vilivyo na alama ya CHadema viliuzwa jijini Arusha kwa wingi.
Mke wa Mbunge Godbless Lema akiwa kwenye gari pamoja na mtoto wao wakati wa mapokezi hayo.
Lema Arusha anafananishwa na Barack Obama
Watu walining'inia katika magari bila hofu
Huyu na e'eti' alikua anachukua kumbukumbu za Video....
Lemna akiwa na Mbunge wa Arumeru Mashuari CHADEMA, Joshua Nasari.
MAPOKEZI ya Kihistoria katika jiji la Arusha yamefanyika leo wakati
wafuasi, Mbunge wa Arusha Mjini kwa Tiketi ya Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Godbless Lema walipo miminika kwa Wingi kuanzia
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) hadi katika Viwanja
vya Kilombero mjini hapa alipohutumia maelfu ya wana CHADEMA Arusha
Mjini.
Mapokezi yahoo yamefanyika wakati Godbless Lema alipokuwa akirejea mjini
Arusha akitokea jijini Dar es Salaam kusikiliza hukumu ya Rufani ya
Keshi yake ya Kuvuliwa Ubunge iliyotolewa maamuzi ya kumrtejeshea Ubunge
wake Desemba 21,2012
Post a Comment