MATOKEO YA KIDATO CHA NNE LEO

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Philipo Mulugo

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatarajia kutangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana.
  Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Philipo Mulugo, aliiambia NIPASHE katika mahojiano jana kuwa taratibu zote kwa ajili ya kutangaza matokeo hayo zimekwisha kukamilika na sasa yatatangazwa rasmi leo. 
Wiki iliyopita Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa, akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza ajira mpya za walimu aliahidi kuwa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yatangazwa mwishoni mwa wiki hiyo, lakini hata hivyo hayakutangazwa.
  Dk. Kawambwa ambaye aliulizwa ni kwa nini matokeo ya mtihani huo yanacheleweshwa kutangazwa ukilinganisha na miaka ya nyuma, alisema kimsingi hayajachelewa kwa sababu wanafunzi watakaochaguliwa kuingia kidato cha tano wanatakiwa kuripoti mwezi Julai mwaka huu. 
  “Kila mtu anauliza suala la matokeo, kimsingi hatujachelewa sababu hata wanafunzi watakaochaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano watajiunga mwezi Julai, Mungu akipenda yatatangazwa kabla ya Jumamosi,” alisema Dk. Kawambwa.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments

Powered by Blogger.