PICHA: SHULE YA MSINGI MEDELI ILIYOKO MANISPAA YA MJI WA DODOMA MPAKA LEO WANAFUNZI WANAKAA CHINI

Shule ya msingi Medeli imechakaa pamoja na kuwa mjini waheshimiwa wanaingia na kutoka, watoto wanakaa chini, matundu ya vyoo ni 6 kati ya wanafunzi 789 hivi kweli haya ndio maisha bora kwa kila mtanzania?
 Wanafunzi wa shule ya msingi Medeli iliyopo kata ya Tambukaleli manispaa ya Dodoma wakiwa wamekaa kwenye mifuko ya salfeti iliyotandikwa chini kutokana na shule hiyo kukosa madawati tangu mwaka 2007 ilipojengwa.(Picha na John Banda)
 Muonekano wa jengo la shule hiyo kwa nje ambalo uchakavu wake kwa ndani kutokana na kutosakafiwa kwa muda mrefu unatisha zaidi kutokana na wanafunzi kukaa chini kwenye vumbi jingi hali ambayo ni hatari kwao kiafya.
Wanafunzi wa Shule ya msingi Medeli kata ya Tambukaleli wakicheza mpira uliotengenezwa na vitambaa kutokana na shule hiyo kukosa vifaa vya michezo kama ilivyo kwa shule nyingine hali inayochangia kwa kiasi kikubwa michezo kushuka shuleni hapo.

No comments

Powered by Blogger.