ABIRIA WANUSURIKA KIFO KWENYE BASI LA SAI BABA BAADA YA KUPASUKA TAIRI


Basi likiwa chini  ya daraja baada ya kupasuka njia na kuacha njia
Basi liliweza kusimama salama na hakuna mtu yeyoye aliyejeruiwa katika ajari hiyo( Picha na Michuzi Blog)

ABIRIA wapatao 45 waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya Sai baba,kutoka Jijini Dar  es salaam kwenda Masasi,mkoani Mtwara,wamenusulika kifo,kufuatia gari yao kuacha njia na kutumbukia mtoni.

Tukio la ajali hiyo limetokea maeneo ya kijiji na kata ya Mbanja,iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
Katika ajali hiyo watu watano akiwemo dereva na kondakta ndiyo waliokuwa wameumia na kukimbizwa Hospitali ya mkoa ya Sokoine kwa matibabu.

Waliojeruhiwa ni,Juma Mtoi (Dereva),Said Mkumbwa (Kondakta) wakazi wa Jijini Dar es salaam,na kwa upande wa abiria ni John Kasawala (21),mkazi wa kijiji cha Nangamba,wilaya ya Nanyumbu,mkoani Mtwara,Noel Akui (35) mkaazi wa wilaya ya Masasi,mkoani Mtwara na Kuruthumu Ally (25) wakazi wa mji wa Lindi.

Said Mkumbwa ambaye ni kondakta wa basi hilo, amesema kwamba chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka kwa tairi la mbele upande wa kulia kwa dreva, ambapo liliacha njia na kutumbukia mtoni chini ya daraja la
Mbanja. Akasema basi lake lililokuwa limebeba abiria 45 lilikuwa likitoka Jijini Dar es salaam kuelekea wilaya ya Masasi,mkoani Mtwara,kufuatana na ruti zake.

“Tulikuwa tikitokea Dar es salaam kwenda Masasi,kwani ndiyo ruti yetu ilivyo, na ndipo tulipofika eneo hilo mpira wa tairi ya mbele upande wa dereva likapasuka na kukosa mwelekeo kisha likagonga kingo ndogo ya
daraja na kutumbukia mtoni,,,,,,,,,tunachoshukuru ni kwamba wote tumetoka tukiwa hao hakuna aliyepoteza maisha”Alisema Mkumbwa.

Kuruthumu Ally ambaye amepata michubuko kiasi usoni na mabegani na John Kasawala aliyeumia kichwani,kwa nyakati tafauti walisema wao walikuwa wamekaa sehemu ya mbele na ghafla walisikia mlio mkubwa kisha basi lao kuyumba na kutumbukia chini ya daraja.

Akizungumza kwa niaba ya kaimu mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo,Dkt,Edgar Mlawa amesema majeruhi hao wameumia sehemu mbalimbali ya miili yao,ikiwemo vichwani na hali zao zinaendelea vizuri na kuna mategemeo ya kuweza kuendelea na safari zao kama kawaida.

“Hapa Hospitalini wamefikishwa majeruhi watano tu,akiwemo dereva,kondakta wake na abiria watatu,mmoja wao ni mwanamke, ambapo wote hao hakuna aliyekuwa sirias kwa kuumia licha ya kupata majeraha sehemu mbalimbali ya miili yao.ikiwa ni pamoja na vichwani”Alisema Dkt,Mlawa.

No comments

Powered by Blogger.