ZAIDI YA NGOS 1000 KUFUTIWA USAJILI NCHINI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu. 


Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali anatarajia kuyafutia usajili zaidi ya Mashirika 1000 kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria katika utendaji kazi wake tangu yasajiliwe.

 Hatua hiyo inatokana na maelekezo ya Bodi ya Uratibu ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali katika kikao chake kilichofanyika hivi karibuni mkoani Geita. 

Kufutwa kwa mashirika tajwa kunatokana na kushindwa kutoa taarifa zake za kila mwaka kama inavyosisitizwa na sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24, 2002 hali inayosababisha kazi za mashirika hayo kutofahamika vyema na hivyo kukosa sifa ya kuendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria. 

Orodha ya Mashirika tajwa itatolewa kwa umma hivi karibuni na inahusisha pia Mashirika ya Kimataifa.


CHANZO: MICHUZI BLOG


No comments

Powered by Blogger.