TEMEKE MABINGWA WA PROIN WOMEN TAIFA CUP MARA BAADA YA KUIFUNGA PWANI KATIKA FAINALI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo, Mh Dkt Femella Mukangara (wa pili kushoto) akiwasili katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi wakati wa fainali ya Mashindano ya Proin Women Taifa Cup yaliyofikia Tamati leo kwa kuzikutanisha Timu za Temeke na Pwani.
Waziri wa habari utamaduni na Michezo, Mh Dkt Fenella Mukangara akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya Temeke mara baada ya kuibuka washindi wa Mashindano ya Proin Women Taifa Cup ambayo yalichezwa katika Dimba la Azam huku Proin Promotions na Azam wakidhamini mashindano hayo.

Nahodha wa Timu ya Pwani akipokea Mfano wa hundi ya Shilingi Milioni Mbili ambazo ni zawadi ya Mshindi wa pili katika Mashindano ya Proin Women Taifa Cup na kuwamalizika kwa Temeke kuwa Mabingwa kwa kuifunga Pwani goli 1 kwa 0.
Nahodha wa Timu ya Ilala ambao ni washindi wa tatu akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni 1 ambayo mshindi wa tatu katika Mashindano hayo ni Ilala
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara (wa kwanza kulia) na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Jamal Malinzi wakishuhudia fainali ya Mashindano ya Proin Women Taifa Cup mechi iliyochezwa katika dimba la Azam Complex kwa kuzikutanisha timu za Pwani na Temeke na Temeke Kuibuka Bingwa wa Proin Women Taifa Cup kwa kuichapa Pwani goli 1 kwa 0.
Kikosi cha Timu ya Pwani
Kikosi cha Timu ya Temeke ambacho kimeifunga Kikosi cha Timu ya Pwani kwa goli 1 kwa 0 katika Mchezo wa Fainali ya Mashindano ya Proin Women Taifa Cup, mchezo uliomalizika kwa Temeke kuibuka mabingwa wa Proin Women Taifa Cup katika Dimba la Azam Complex
 Waziri Mukangala akisalimiana na timu ya Temeke pamoja na timu ya Pwani kabla ya Mechi ya Fainali ya Proin Women Taifa Cup kuanza katika dimba la Chamanzi Complex. Temeke iliibuka Mshindi kwa kuifunga Pwani Goli 1 kwa 0
Hatari langoni mwa timu ya Pwani
 Wakichuana vikali
Wachezaji wa timu ya temeke wakishangilia goli lililofungwa katika kipindi cha Kwanza cha Mchezo na kupelekea kudumu kwa dakika tisini na kuwapa ubingwa temeke.
 Mashabiki waliojitokeza kushuhudia mtanange huo 
 Mlinda mlango wa timu ya Temeke akiokoa moja ya hatari iliyopelekwa katika lango lake
 
 Wachezaji wa Pwani wakisikitika kwa kufungwa na Temeke
Picha zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

No comments

Powered by Blogger.